Ikiwa umeumizwa na maneno au matendo ya mwenzi wako, je, unaweza kumsamehe? Ikiwa huwezi, usiamue kumnyamazia tu. Ongea na mwenzi wako kwa utulivu bila kukawia, ikiwezekana siku hiyohiyo(kununa au kususa haisaidii).
Uwe na matarajio halisi
Mkipatwa na dhiki,misukosuko ya kifamalia msiamue haraka-haraka kwamba mlikosea kuoana. Badala yake, shirikiana na mwenzi wako kutatua matatizo na mwendelee “kuvumiliana na kusameheana kwa hiari.
Ishi kulingana na nadhiri yako ya ndoa

Je, unakumbuka maneno ya nadhiri yako ya ndoa? Kwa nini usiyatafakari tena na ujiulize: ‘Je, ninatimiza ahadi yangu?’ Usifikirie sana jinsi mwenzi wako anavyotimiza nadhiri yake. Nadhiri yako ilikuwa na maneno ambayo wewe ulisema ungefanyaIkiwa kila mmoja wenu atazingatia kutimiza nadhiri yake, inaelekea kwamba nyote mtafurahia matokeo,hapa kwenye ahadi wengi wameweka kama fashioni tu na sisi watazamaji unapokuwa unasema yale maneno tunaamini kuwa huyo ndo umemchagua na ulikuwa makini katika hilo, tuishi kulingana na nadhiri zetu na ndoa zitadumu
****************************** *************
Karibuni kwa michango zaidi